Wednesday 20 April 2016

TETESI ZA MOURINHO KUELEKEA UFARANSA.

Tetesi za Mourinho kuelekea Ufaransa


Kocha Jose Mourinho adaiwa kufanya mazungumzo na kilabu ya PSG nchini Ufaransa
Baada ya kimya kirefu tangu kutimuliwa Chelsea, tetesi mpya zimeanza kuibuka kuhusiana na kocha Jose Mourinho ambaye kwa sasa hana timu.


Kwa mujibu wa taarifa zilizochapishwa na vyombo vya habari vya Uingereza, kocha Mourinho anadaiwa kufanya mazungumzo na kilabu ya PSG nchini Ufaransa.


Katika siku za hivi karibuni, Mourinho pia amekuwa akihusishwa na tetesi za uwezekano wa kupewa fursa ya kuchukuwa nafasi ya Louis van Gaal na kuinoa Manchester United nchini Uingereza.


Tangu mwaka 2013, kilabu ya PSG imekuwa chini ya mkufunzi Laurent Blanc ambaye ameiwezesha kunyakuwa mataji 9.


Mourinho mwenye umri wa miaka 53 aliwahi kuwa mkufunzi wa Porto, Inter, Real Madrid na Chelsea.

 
Licha ya tetesi hizo kugonga vichwa vya habari, kilabu ya PSG bado haijatoa maelezo yoyote kuhusiana na madai hayo.

No comments: