Monday 11 April 2016

KVZ YAKOMAA MBELE YA KMKM.



Timu ya Kikosi  Maalum cha Kuzuia Magendo KMKM imekubali kubamizwa kichapo cha mabao 2-0 walipocheza na Kikosi cha Valantia Zanzibar KVZ katika mchezo wa ligi kuu ya Zanzibar kanda ya Unguja.
Mchezo huo uliovurumishwa ndani ya uwanja wa Amani majira ya saa kumi za jioni, KVZ waliutawala mchezo huo na kuwazidi KMKM takriban dakika zote za mchezo, na KMKM hawakuoneka kabisa kucheza katika mtanange huo.

Mabao ya KVZ yamewekwa kimyani na Salum Songoro katika dakika ya 35, na bao la pili limefungwa na Suleiman Hassan mnamo dakika ya 89 ya mchezo huo.

Kocha wa KMKM Ali Bushir Mahmoud amesema kuwa wachezaji wake hawakucheza kama alivyowafundisha.

“Mchezo wa leo tumepoteza kwa kweli wachezaji wangu wameniangusha, sijawahi kusema kitu icho lakini nathubutu kusema kwamba vijana wangu wameniangusha kwa sababu kipindi ambacho tulikuwepo katika matayarisho ya mchezo huu tulifanya mabo mengi sana ambayo leo sikuona hata moja katika yale ambayo tumefanya hawakufanya kabisa wamecheza mpira sio kabisa, sasa nathubutu kusema kwamba wachezaji wangu wameniangusha kabisa”. Alisema kocha Bushiri.

“Nimepata ushindi ambao sikuutegemea kwa sababu mechi ya kwanza KMKM waliweza kunifunga kwa mabao 2-1 kwa hiyo leo nimekuja kwamba vipi nitaweza kupigana na timu ya KMKM na nashukuru Mungu kwamba nimeweza kushinda mabao 2-0”. Alisema kocha King.

Matokeo hayo yameifanya KVZ kuwa na alama 33 na kubaki nafasi yao ya pili, huku KMKM wakibaki nafasi yao ya nne na alama 27.

No comments: