Monday 11 April 2016

WAZAZI PUNGUZENI PINGAMIZI KWA WATOTO.


WAZAZI wametakiwa kuondoa dhana potofu ya kwamba mwanafunzi akishiriki michezo Skuli hushusha kiwango cha ufahamu wa masomo yake  darasani .

Mratibu wa michezo Wilaya ya Micheweni mwalimu Ali Nassor amesema kuna uhusiano mkubwa kati ya elimu na michezo kwani  michezo hukuza kipaji cha mwanafunzi

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi , mwalimu Ali amewataka wazazi kuondoa vizuizi kwa watoto wao bali wawape fursa na muda wa kutosha kushiriki michezo .

Aidha amefahamisha kwamba watoto wengi wamepata ajira kupitia michezo , na kuwaeleza kuwa kuna tofauti kubwa ya ufahamu wa mwanafunzi ayeshiriki michezo na asiye shiriki michezo .

Mwalimu Ali pia amewasisitiza wazazi kujenga utamaduni wa kufuatilia maendeleo ya watoto wao , na kuacha kukaaa majumbani na kutupa lawama wa walimu na kamati za skuli pekee.


Naye mwalimu Zawadi Amour Nassor amesema kuwa walimu wameandaa ratiba ambayo itamfanya mwanafunzi kushiriki michezo bila ya kuathiri ratiba ya vipindi vyake vya masomo darasani .

No comments: