Waziri Mbalula alisema
kuwa serikali haitaruhusu kamwe uwenyeji wa mashindano hayo manne kwa sababu
yameshindwa kutekeleza matakwa yao kikatiba kuongeza idadi ya wachezaji weusi
katika timu za taifa.
Kauli hiyo ni pigo
kubwa kwa shirikisho la raga la Afrika Kusini kwani ilikuwa imepanga kuwania
uwenyeji wa mashindano ya dunia ya mwaka wa 2023.
Mwandishi wa BBC nchini
humo anasema kuwa zaidi ya miongo miwili tangu kumalizika kwa utawala wa
wazungu nchini Afrika Kusini, mashirika ya michezo nchini humo mara nyingi
hulaumiwa kwa kuwa na wazungu wengi kuliko wachezaji weusi.
Aidha Mbalula amekuwa
akiishawishi shirikisho hilo la raga kuwakuza wachezaji weusi bila mafanikio.
Mashirikisho hayo
makubwa ya michezo nchini humo yalitia sahihi mkataba wa kuimarisha idadi ya
wachezaji weusi mwaka wa 2014 hata hivyo kufikia sasa ni shirikisho la kandanda
pekee lililotimiza matakwa hayo.
Hii inamaanisha kuwa
mashirikisho hayo manne hayataruhusiwa kuandaa ama hata kuwania uwenyeji wa
mashindano yeyote ya kimataifa.
Kamati maalum itakutana
mwishoni mwa mwaka wa 2018 kutathmini maendelea ya mashirikisho hayo manne.
Marufuku hiyo hata
hivyo haitaathiri uwenyeji wa michezo ya jumuiya ya madola ya mwaka wa 2022
ambayo imeratibiwa kufanyika mjini Durban Afrika Kusini
No comments:
Post a Comment