Mahrez amefunga mabao
17 na kusaidia katika ufungaji wa mengine 11 katika mechi 34 za ligi
alizochezea Leicester na kuwasaidia sana kukaribia kushinda taji la ligi.
Mahrez ni raia wa
Algeria.
Wachezaji soka ya
kulipwa Uingereza ndio hupiga kura kuamua mshindi.
Kiungo wa kati
Tottenham Dele Alli, mwenye umri wa miaka 20, ndiye aliyeshinda tuzo ya PFA ya
mchezaji chipukizi wa mwaka naye mshambuliaji Izzy Christiansen akashinda tuzo
ya mchezaji bora wa kike wa mwaka.
Mshambuliaji wa
Sunderland Beth Mead, mwenye umri wa miaka 20, ndiye aliyeshinda tuzo ya
mchezaji bora chipukizi wa kike.
No comments:
Post a Comment