Nusu fainali ya kwanza ya kombe la FA nchini
Uingereza ilichezwa kati ya Manchester United na Everton katika uga wa Wembley.
Timu hizo mbili zilitoana jasho ili kuwania nafasi
kwenye fainali ya kombe la FA.
Manchester United ilitangulia kupata goli la kwanza
lililofungwa na Fellaini katika dakika ya 34 kabla ya beki wao Chris Smalling
kujifunga katika dakika ya 76 na kusawazishia Everton.
Baada ya vuta nikuvute ya dakika za mwisho,
Manchester United ilifanikiwa kupachika goli la pili kupitia Anthony Martial
aliyefunga katika dakika ya 90 na kuihakikishia ushindi.
Sasa Manchester United itasubiria mpinzani wake wa
fainali ya kombe la FA atakayebainika hapo kesho kati ya Crystal Palace na
Watford.
No comments:
Post a Comment