Real Madrid yaicharaza Rayo Vallecano 3-2 kwenye mechi ya La Liga.
Timu ya Real Madrid
ilisafiri ugenini kutoana jasho na Rayo Vallecano kwenye mechi ya ligi kuu ya
soka ya La Liga nchini Uhispania.
Wenyeji Rayo Vallecano
walianza vyema mechi hiyo na kutangulia kupata bao 2 zilizofungwa na Embarda
katika dakika ya 7 na Miku katika dakika ya 14.
Licha ya kuonyesha
mchezo mzuri, Rayo Vallecano walishindwa kukizuia kikosi cha mashambulizi cha
Real Madrid na kukombolewa magoli yote na kuongezwa la tatu.
Gareth Bale aliifungia
Real Madrid magoli mawili huku Lucas Vazquez akifunga moja na kuipa timu ya
ushindi wa 3-2.
No comments:
Post a Comment