Mabingwa wa raga nchini
Kenya watunukiwa shilingi Milioni 10 na rais Uhuru Kenyatta
Siku ya Alhamis rais wa
Kenya Uhuru Kenyatta alikuwa mwenyeji wa washindi wa timu ya kitaifa ya mchezo
wa raga katika ikulu ya rais mjini Nairobi.
Mabingwa hao wa Kenya
Sevens Rugby walirudi nchini Kenya siku ya Jumanne baada ya kuibuka washindi
katika michuano ya raga roundi ya nane ya mchezo wa raga HSBC World.
Nahodha wa timu hiyo ya
kitaifa Andrew Amonde alimkabidhi rais Uhuru kombe la ushindi .
Akitoa hotuba yake
wakati wa hafla hiyo,rais Uhuru Kenyatta alitangaza tuzo la shilingi milioni 10
kwa timu hiyo kutoka kwa serikali ya Kenya kama shukrani kwa mashujaa hao kwa
kuendelea kupeperusha bendera ya Kenya Kimataifa.
Aidha mbali na tuzo
hilo rais Kenyatta aliongezea kuhakikishia kuwa udhamini wa timu hiyo
utaendelea kuimarishwa.
Aliambia timu hiyo
waendelee kufanya mazoezi bila ya kuchoka na serikali itaendelea kutoa misaada
ili kutayarisha kuwakilisha nchi katika michezo ya Olimpiki.
No comments:
Post a Comment